Watanzania wenzangu naomba tumsaidie Bi. Sigara apelekwe Hospitali kutibiwa, anahitaji msaada wetu ili aondokane na maumivu aliyonayo.
Anatakiwa kukatwa mkono na kupatiwa matibabu mengine lakini amerudishwa nyumbani kutokana na kukosa pesa.
M-pesa: 0765124141 Rehema Mahenge
Habari Tanzania 🇹🇿 neno langu la asubuhi hii, natamani Ubunge nao uwe na kikomo cha awamu mbili kama ilivyo Urais, tunahitaji kupata mawazo mapya ili kuleta chachu ya maendeleo.
Inadaiwa
@Eng_Matarra
yuko jela kutokana na makosa ya kimtandao. Tunahitaji kushirikiana kwa pamoja kupata taarifa zake ili tuweze kumtoa gerezani.
Bado hatujachelewa🙏
Watanzania wenzangu kama tunaweza kupata namba ya mke wa
@Eng_Matarra
au ndugu ambaye inadaiwa kafungwa jela miaka 10 itapendeza zaidi ili tujue tunaanzia wapi na kwanini alifungwa.
Umoja ni nguvu tusimuache mwenzetu huko, tujaribu kama tunaweza mtoa
@TitoMagoti
@PMadeleka
Nimefikiria maumivu ya mama huyu nimeshindwa kuyabeba, amegundua mabinti zake walioko chuo kumbe wana watoto zaidi ya umri wa mwaka 1 na hajui.
Watoto walikuwa wanasoma chuo Dar hawarudi likizo akajua wanaenda kwa ndugu zao.
Hadi sasa mama huyu hali yake ya kiafya sio nzuri.
Humu tunachati na watoto sana ambao wengine hata hawajui maisha nini, hawana majukumu na bado wanategemea kulishwa ndiyo maana wanachowaza wao ni kutrend na matusi tu.
NEC sijawaelewa kabisa yani mtu ana LESENI anaruhusiwa kupiga kura? kuna uhakika gani kama ni halali? kuna utaratibu gani uliowekwa kupitia LESENI hizo kabla ya kupiga kura? Nina maswali mengi sielewi🤔
WE DID IT, FAMILY 🙌🏿🔥🔥🔥
Tumefikia lengo na zaidi.
Lipa Namba: 2,800,000
Mpesa: 4,400,000
Jumla = 7,2000,000
Kesho tutatoa taarifa ya mrejesho wa kulipa faini na kumtoa Matara gerezani.
Mungu awabariki🙏
#Justice4Matara
Nyie kuwa Mwanaharakati inahitaji moyo sana, leo nilikuwa kibamba ndani huko kufatilia kesi ya ukatili, vibaka walitaka kunipora simu ikabidi nijidekeze na kujifanya msela wao, ni vijana wadogo wanavuta bangi na wanakunywa pombe kali aisee, hapo ni sehemu ambayo ni bondeni.
Mtoto wa darasa la 7 amekunywa sumu na kupoteza maisha baada ya kugundua dawa anazokunywa kwa muda wote ambazo anapewa na mama yake ni kwa sababu yeye ni muathirika wa UKIMWI.
TAARIFA YA MAKUSANYO YA MCHANGO WA MATARA
Makusanyo: 10,030,000
Matumizi: 5,210,000
Kiasi kilichobaki: 4,820,000
Pesa iliyobaki atatutumiwa Matara.
Asanteni nyote. Mbarikiwe sana🙏
Habari
@CrownMediaTZ
Lengo la twit hii ni kuomba nafasi katika kipindi hiki cha michezo naona hakina mwanamke ili kuongeza ladha zaidi.
Mimi sio maarufu lakini nina ujuzi katika tasnia ya habari hususani kipindi cha michezo. Asante
Wako katika ujenzi wa taifa
Devota Tweve 😅
Kuhusu tumelipa faini shingapi, fedha iliyobaki na matumizi yote tutatoa update, Asante kwa kuniamini katika hili mmeonyesha upendo ambao kibinadamu hauelezeki.
Tubarikiwe sote🙏
Mitandao ya simu imekuwa ikitunyonya wateja wake, kuleta usumbufu na kujipatia faida kwa kutoa namba zetu kwenye kampuni mbalimbali ambazo zimekuwa zikituma matangazo yao kwetu bila idhini yetu.
Hili halitakiwi kufumbiwa macho maana wanakera sana.
Me Devotha Tweve natangaza nia ya kugombea Ubunge 2020 katika jimbo 1 linalopatikana mkoani Songwe, naamini chama changu kitanipa ridhaa ya kuwania kiti hiki ili nitatue changamoto wanazozipitia vijana wenzangu na jamii kwa ujumla, naombeni sapoti yenu😃
#IWD2020
#EqualforEach
UPDATE:
Jitihada za kulipa faini ya Japhet Matarra hazijafua dafu leo.
Leo tumekwama kurejesha faili kutoka Mahakama ya Rufani kurudi Wilaya.
Kesho Mawakili wataendelea na kazi na tuna imani suala hili litakamilika.
Kazi nzuri sisi sote.
#JusticeForMatarra