Nimesikiliza Bonge wa PB anaongea na wale kina mama wanaofanya kilimo cha mchicha pembeni ya ubalozi wa Marekani kuwa walinyimwa maji ya Dawasco ikabidi waombe msaada ubalozini na benki ya dunia wakachimbiwa kisima. Nimehisi aibu aise..
Mr Kuku kuna watu waliambiwa mchongo utaisha vibaya wakabisha kama ambavyo hizi mambo za forex na bitcoin zinavyoshobokewa sasa hivi.
Sema tusichoke kukumbushana kwamba hakuna shortcut kwenye kutafuta hela, na mtu anapokulisha maneno matamu kuhusu fursa jua wewe ndo fursa.
Sidhani kama kuna kampuni ina mfumo mzuri wa kufuatilia wateja kama DStv, kuna wakati nilisusa kulipia mtu wao akaniuliza kama kuna tatizo nikamwambia mpaka Solkjaer afukuzwe kazi, siku mbili baada ya Rangnick kuajiriwa yule dada akanipigia kukumbushia 😂
All Hail Faustine of House Ndugulile, first of his name, rightful leader of Kigamboni, Conqueror of Kura za Maoni, Destroyers of zeroes. A leader at heart.
#Ndugulile5Tena
Umemaliza kula zako mtori na chapati mbili kijasho kinakutoka unasubiri mhudumu akuletee maji makubwa, mara askari polisi anaku-arrest kwa sababu unaonekana una dalili za kutaka kujinyonga 😂😂
Hivi wanamuziki wanawezaje kuimba au kuchana masaa mawili mfululizo bila sauti kukauka wakati kina sie kushangilia dakika 15 tu ukikatiza kawe ukaongea gizani wanajua mbunge wao? 🤦🏿♂️🤷🏿♂️
JE WAJUA
Shilingi milioni 45,817,013.81 ($20,000) hutumika kwa siku moja tu kumlinda muasisi wa Facebook Mark Zuckerberg. Inatajwa bajeti ya $7,326,640 (Sh 16,782,594,507) imetengwa kwa ajili ya ulinzi wa Zuckerberg na familia yake kwa mwaka
#ElimikaWikiendi
Utamsema Kiba kwenye kitu chochote ila sio utunzi. Jamaa ni fundi, hakuna kuunga unga maneno hadi kuchanganya majina ya vyakula ili wimbo wa mapenzi uvutie kuusikiliza.
Abdul Nondo anatema nondo Clouds360 hadi Sam Sasali kakaa kimya mazungumzo ni back and forth ya Babie na Abdul, kuna mwingine wa NCCR ndo kama vile anachukua notisi
Power Breakfast leo walikuwa Kariakoo na wafanyabiashara watatu; Mkinga, Mchaga na Mpemba. Kuna muda wakawaambia kila mmoja ataje sifa moja anayoikubali na kujifunza kwa mwenzake, matokeo:
Mpemba - Uaminifu
Mchaga - Upambanaji (Aggressiveness)
Mkinga - Nidhamu kali ya fedha
@mpambazi
Mtu wangu wa nguvu nimekusogezea dondoo kadhaa za namna ya kupata mtaji maana hawa uliowaita “mahanisi” sidhani kama watakuwa na msaada kwakk
Punguza munkari, kumbuka:
- Umezaliwa nchi ambayo mafua yapo kila aina, kuna ya vumbi, mvua/baridi hadi hewa chafu na hayajakuua.
- Hakuna Mwafrika aliefariki, hata waliokuwa Wuhan wamewashangaza Wachina
- Kirusi cha Corona kinaogopa joto, wagonjwa wote Afrika wanapona fasta
Nimekuta mtu ka-park vibaya katublock karibu nusu saa nzima, nilikuwa nimeshajiandaa kumwaga nyongo mara kaja mwenyewe kumbe ni kiumbe mzuriiii ana unywele mkali. Nimeishia kuwa mlaini kama mkate wa bakhresa kwenye chai ya uvuguvugu. Nawaomba radhi mababu zetu Adam na Samson.
Ukiangalia HARDtalk ya Lissu unagundua umuhimu wa waendesha vipindi kuwa na timu ya kufanya research kabla ya kumhoji mtu. Utasema mtangazaji anafuatilia siasa za Tanzania au kawahi kuishi bongo.
"Hauwezi kuondoa umaskini wa nchi hii & kuleta mapinduzi ya viwanda bila kuwekeza kwenye kilimo"
"Hauwezi kukamua maziwa ng'ombe usiemlisha" -
@HusseinBashe
Inawezekana Makalla hajui kuwa kuna maeneo ya Dar abiria analazimika kulipa gharama ya bajaji au boda inayokaribiana na nauli ya kwenda mkoani ili awahi bus la kwanza alfajiri, wenye mabasi wanafanya kutusaidia kushusha na kupakia maeneo kama G/mboto, Kigamboni na Mbagala.
Kama moja ya malengo yako 2019 ni kujitahidi kusafiri kwa kutembelea vivutio vya ndani lakini huna kampani au gharama zinakukatisha tamaa, tafadhali tuwasiliane tuone namna gani tunakuwa na group la wanaosafiri pamoja kwa gharama nafuu. DM iko wazi.
Miezi mitatu au minne hii iliyopita social media imefanya nigundue kuna uchafu mwingi sana unaendelea kwenye hizi shule za mtaala wa nje, na inaonekana wazazi wengi hawajui au wanashtuka tu kuona confession kwenye social media.