Mchimbaji Mdogo wa Madini Mkoani Shinyanga ameuza Almasi yake kwa Tsh. Bilioni 3. Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo ashuhudia. Serikali yapata Milioni 238 kutokana na mauzo hayo.
Afisa Madini akionyesha moja ya jiwe la Tanzanite alilopata mchimbaji mdogo wa Madini ambapo amepata mawe mawili yenye thamani ya Sh. bilioni 7.8.
Leo Wizara inamtambua rasmi mchimbaji huyo Bw. Laizer kuwa bilionea.
STAMICO imeanza Ujenzi wa Mtambo wa Kusafisha Dhahabu jijini Mwanza chini ya Kampuni ya Mwanza Precious Metal Refinery Company Limited.Mtambo huo utakamilika Desemba2020 na utakuwa na uwezo wa kusafisha zaidi ya kilo 480 za dhahabu kwa siku kwa viwango vya kimataifa 99.99%Purity
Waziri wa Madini Angellah Kairuki leo Oktoba 24, amefungua Jukwaa la Sekta ya Uziduaji Tanzania.
Jukwaa hilo limeandaliwa na Mtandao wa Asasi za Kiraia (HAKI RASILIMALI) unaofanya kazi za Uchechemuzi katika Sekta ya Uziduaji Tanzania.
"Kabla ya Kujengwa Ukuta tulikuwa tunapata asilimia 5 tu ya Tanzanite asilimia 95 ilikuwa inatoroshwa. Tuliamua kujenga ukuta ili tumwone kila anayeingia na kutoka," Waziri wa Madini, Doto Biteko.
Ujue Mgodi wa Dhahabu wa Biharamulo(STAMIGOLD) unaomilikiwa na kuendeshwa na Watanzania kwa Asilimia 100.Mgodi huu ni Kampuni Tanzu ya STAMICO. Katika Kipindi Cha Julai2019-Februari 2020 ulizalisha na kuuza wakia 9107.45 za Madini ya Dhahabu na wakia 1,170.21 za Madini ya Fedha
Mawe Makubwa Mawili ya Tanzanite moja likiwa na uzito wa kilo 3.74 na jingine likiwa na uzito wa kilo 1.48 yamepatikana ndani ya machimbo ya Tanzanite Mirerani kutoka kwa mchimbaji mdogo, Anselm Kawishe.Mawe hayo yanatarajiwa kununuliwa na Serikali kwa shilingi 2,245,571,543.46
Waziri wa Madini Doto Biteko amezindua Viwanda Viwili vya Mfano vya Uchenjuaji Madini ya Dhahabu vya Katente- Bukombe na Lwamgasa - Geita na kuvikabidhi kwa STAMICO. Amelitaka shirika hilo kuvisimamia ipasavyo kwa kuwa Serikali imetumia gharama kubwa katika ujenzi wake.
Jengo Jipya litakalotumiwa na Wafanyabiashara wa Madini Mkoani Geita .Jengo hili limejengwa kwa Fedha za Huduma kwa Jamii (CSR) zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) na kusimamiwa kwa ushirikiano baina ya mgodi huo na Halimashauri ya mji wa Geita.
Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko ametembelea Mgodi wa Dhahabu wa Busolwa Mining Limited unaomilikiwa na Mtanzania Wilayani Misungwi Mkoa wa Mwanza. Amepongeza kwa uwekezaji mkubwa na wa kisasa uliofanyika ikiwemo kutoa ajira zipatazo 127 kwa watanzania.
Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko amefanya ziara ya kushtukiza katika Mgodi wa Dhahabu wa MMG unaomilikiwa na Kampuni ya Waarmenia uliopo katika Wilaya ya Musoma, Mkoani Mara na kubaini raia wa kigeni 10 wasio na vibali vya kazi waliokuwa wamejificha ndani ya mgodi.
"Tuna kazi nyingine kuhakikisha uongezaji Thamani Madini unafanyika hapa nchini ikiwemo kuongeza maeneo mbalimbali ya shughuli hizi. Kwa upande wa Serikali tayari tumeendelea kukiimarisha Kituo chetu cha TGC kinachotoa mafunzo ya uongezaji thamani,' Waziri Biteko.
#Ajira
Waziri wa Madini Angellah Kairuki leo Oktoba 17, amempokea Waziri wa Madini kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ( DRC), Martin Kabwelulu pamoja na Ujumbe wake ambao wamefika kwa lengo la kujifunza kuhusu Mabadiliko ya Sheria ya Madini na kubadilishana uzoefu.
Tayari Viongozi mbalimbali wamewasili katika eneo la tukio kwa ajili ya kushuhudia Serikali ikikabidhiwa Jiwe lingine la Tanzanite lenye Uzito Mkubwa wa Kilo 6.33 kutoka kwa Mchimbaji Mdogo wa Madini ya Tanzanite, Saniniu Laizer. Tukio hili litarushwa Mubashara.
#NiLaizerTena
Usikose kufuatilia mubashara kupitia TBC1, ITV, CHANNEL TEN, CLOUDS TV, TVE na mitandao mbalimbali ya Kijamii, Hafla ya Utiaji Saini Mikataba baina ya Serikali na Kampuni za Uchimbaji Madini kuanzia saa Tatu Asubuhi leo Desemba 13, 2021
@Tumeyamadini
@STAMICOTZ
@TZMsemajiMkuu
MABADILIKO
Hafla ya Serikali kupokea Gawio kutoka Kampuni ya Madini ya Twiga na Shirika la Madini la Taifa ( STAMICO) Iliyokuwa ifanyike Ikulu Jijini Dar Es Salaam, itafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Saa 8:00 Mchana
@TZMsemajiMkuu
@maelezonews
"Kabla ya kwenda Kwenye Box la Kura Mwaka huu tutafungua Migodi Mipya Miwili ya Uchimbaji wa Kati. Mmoja wa Graphite Ruangwa na mwingine wa Madini Mazito ya Baharini (Heavy Mineral Sand), Kigamboni, Jijiji Dar es Salaam," Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Prof.Shukrani Manya.
Huu ndiyo Mgodi wa Almasi wa Williamson Diamond Limited ( WDL) uliotaka kuuzwa na Uongozi wa Mgodi huo bila kuitaarifu Serikali ambaye ni Mbia kwa asilimia 25. Upo Mwadui, Wilayani Kishapu Mkoa wa Shinyanga.
#UdhibitiwaRasilimaliMadini
@Tumeyamadini
@serikalikazini
UNAYAJUA MADINI YAPATIKANAYO MKOANI KWAKO? JIPATIE NAKALA YAKO YA KITABU KINACHOONESHA MADINI YAPATIKANAYO KATIKA MKOA, WILAYA, KATA MPAKA KIJIJI KWA BEI NAFUU FIKA KATIKA OFISI ZA GST AU WASILIANA NASI KWA NAMBA 0262323020. KARIBU TUKUHUDUMIE
#lLeoniKagera
@GeologicalT
"Masoko ya Madini yamesaidia kutatua changamoto za muda mrefu zilizokuwa zikiikabili Sekta ya Madini hususan wachimbaji wadogo kukosa masoko ya uhakika na bei stahiki," Waziri wa Madini, Doto Biteko.
Waziri wa Madini Doto Biteko amewataka Wafanyabiashara wa Madini kujiepusha na Vitendo vya Utoroshaji wa Madini kwani Serikali hailali na inafanya kazi usiku na mchana. Amesisitiza utoroshaji madini haulipi. Ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa TAMIDA.
@Tumeyamadini
Tayari Viongozi mbalimbali wamewasili Chuo Cha Madini Kampasi ya Nzega kwa ajili ya Hafla ya Kukabidhi Chuo Madini Kulelewa kwa muda na Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.
Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko ameshuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano kati ya Wizara ya Madini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Maji, Nishati na Madini ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
@maelezonews
@TZMsemajiMkuu
@JamiiForum
@millardayo
Matukio katika picha za uchimbaji na uchenjuaji wa madini ya kinywe (graphite) ktk Mgodi wa GodMwanga Gems Limited unaomilikiwa na Mtanzania. Mgodi huu ni miongoni mwa migodi inayoiweka Tanzania kwenye orodha ya nchi wazalishaji wakubwa wa madini ya kinywe Duniani.
#LocalContent
"Katika kuongeza manufaa yatokanayo na madini muhimu na mkakati, kwa mara ya kwanza kitajengwa kiwanda kikubwa na cha kisasa cha Usafishaji na uongezaji Thamani Madini cha Multi Metals Processing Facility katika eneo Maalum la ukanda wa kiuchumi la Buzwagi Special Economic Zone.
#IGAWIO
"STAMICO ilikuwa ikizalisha madeni hadi shilingi bilioni 63.Hivi sasa Shirika hili halizalishi hasara hata shilingi. Mwaka Jana ilitoa Gawio la Shilingi bilioni 1 mwaka huu limetoa Shilingi Bilioni 1.1 na limepata tenda kubwa ya GGM ya kuchoronga ,"Waziri Doto Biteko
Katibu Mkuu wa Madini Prof. Simon Msanjila leo amekitembelea Kiwanda Cha Kusafisha Dhahabu(Refinery) Cha Eye of Africa kinachojengwa Jijini Dodoma ili kuangalia Maendeleo ya ujenzi wake. Kiwanda hicho ni cha Kwanza cha Kusafisha Madini ya Dhahabu na Fedha nchini.
@serikalikazini
Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko amekamata madini ya vito aina ya Rhodilite yenye uzito wa takribani tani saba yaliyokuwa yamefichwa nyumbani kwa mchimbaji wa madini hayo, Juvenal Mnene ambaye ni mmiliki wa kampuni ya J. J. Mnene & Partners na kuamuru kukabidhiwa Serikalini.
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) inapenda kuwataarifu Watanzania wote kuwa Bilionea Saniniu Laizer atakuwepo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (77) kwenye banda la Tume ya Madini, kuanzia tarehe 12 hadi 13 Julai, 2020.
"Naipongeza sana Wizara kwa kuiwezesha nchi yetu kusafirisha nje Madini ya Bati ( tin) baada ya kupata Cheti cha Uhalisia . Sasa wafanyabiashara wanaweza kuuza madini ya bati nje ya Nchi. Nawapongeza STAMICO kwa kununua bati kutoka kwa Wachimbaji,' Waziri Angellah Kairuki.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof.Idris Kikula ameiagiza kampuni inayojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa matairi ya magari na mitambo ya migodini SuperDoll kuhakikisha inaandaa na kuwasilisha Mpango wa Ushirikishwaji Wazawa (Local Content) kwenye Sekta ya Madini
Bw. Saniniu Laizer mchimbaji aliyepata mawe makubwa mawili ya Tanzanite ambapo moja lina kilo 9.2 ambalo lina thamani ya shilingi bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.
“Kuna biashara nyingi kwenye Sekta ya Madini, hivi karibuni Serikali ya Qatar itaanza kununua dhahabu moja kwa moja kutoka Soko la Geita.” Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila wakati wa kikao chake na Ujumbe wa Benki ya NMB.
Waziri wa Madini Doto Biteko leo ameshuhudia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) likisaini Mkataba wa Kuchoronga Miamba katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita ( GGML) wenye Thamani ya Shilingi Bilioni 5.6 katika kipindi Cha miezi Sita
#StamicoMpya
#FactsandFugures
#TumeboreshaSekta
#MadiniYetuUchumiWetuTuyalinde
" Leseni zote za Madini hutolewa na Tume ya Madini isipokuwa Leseni Kubwa ya Uchimbaji Madini (SML) ambayo hutolewa na Tume ya Madini baada ya kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri," Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mulabwa.
Waziri wa Madini Doto Biteko amekutana na Wawakilishi wa Kampuni ya Jervois Mining Limited ya Australia ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika Mradi wa Nikel-Colbat Kabanga. Waziri Biteko ameendelea kusisitiza kuhusu kufuatwa kwa Sheria na taratibu.
#YafahamuMadiniyaVito
Uthaminishaji wa Madini ya Vito hususan Tanzanite huzingatia ubora ambao huangalia vitu Vinne ambavyo ni Umbo, Uzito, Usafi na Rangi. (4C: Cut, Carat,Clarity& Colour) ambavyo vitapatikana katika jiwe la Tanzanite ambalo litakatwa na kusanifiwa.
#TANZANITE
#UwasilishajiHotubayaBajeti
" Kupitia Masoko ya Madini Wachimbaji Wadogo wamefanya biashara ya madini yenye thamani ya Shilingi trilioni 1.09 na wameingizia Serikali Mapato ya kwa kulipa mrabaha na ada ya ukaguzi ya Shilingi Bilioni 78.01," Waziri wa Madini, Doto Biteko.
#HABARINJEMA
"Kampuni ya Tembo Nickel ambayo Serikali ya Tanzani ni mbia, imepata mafanikio ya kihistoria - kwa mara ya kwanza!
Tembo Nickel kupitia kampuni yake mama ya Lifezone Metals imeandika historia kwa kuzalisha nikeli, shaba, na kobalt," Waziri Anthony Mavunde.
Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema tayari amewasili nchini kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania ambapo amepokelewa na Waziri wa Madini Mhe.Anthony Mavunde.
#Miaka60yaMuungano
Kamishna wa Madini Mhandisi David Mulabwa amepokea Taarifa ya Utafiti uliofanywa katika Tasnia ya Uziduaji ikifungamanisha na Uwekezaji katika Viwanda ikiangazia nchi ya Tanzania. Aliyemkabidhi ni Mkurugenzi Mtendaji wa HAKI RASILIMALI, Rachel Chagonja.
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mjiolojia Fatuma Kyando amesema kuwa madini ya viwanda na madini ya ujenzi yanayochimbwa katika mkoa wa Kilimanjaro yameendelea kupaisha Sekta ya Madini kutokana na ongezeko la wachimbaji wengi wa madini hayo.
@TumeyamadiniTZ
#MafanikioUtekelezajiwaBajeti
Kukamilika kwa ujenzi wa Mgodi wa Mfano wa uchimbaji wa madini ya dhahabu na Mtambo wa uchenjuaji dhahabu kwa wachimbaji wadogo Lwamgasa,Geita.Mgodi huo utasaidia kutoa mafunzo ya namna bora ya uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu kwa wachimbaji wadogo
#Mafanikio
Waziri wa Madini Doto Biteko ameieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuwa mwenendo wa Shirika la STAMICO ni mzuri ikilinganishwa na kipindi cha nyuma na kwamba hivi sasa lina uwezo wa kutoa gawio kwa Serikali la Sh. Bilioni 1.
Naibu Waziri wa Madini Dkt.StevenKiruswa amekutana na kuzungumza & Ujumbe kutoka Marekani uliongozwa &Naibu Waziri wa Nishati wa Nchi hiyoJoshua Volz ambaye ameambatana na viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Nishati ya Marekani &viongozi waandamizi wa Ubalozi wa Marekani nchini
#KikaochaKamatiyaKudumuyaBungeyaNishatinaMadininaWizara
Hadi kufikia Septemba, 2018 kazi ya Ujenzi wa Mgodi wa Mfano Lwamgasa na usimikaji wa mitambo ya uchenjuaji imekamilila kwa asilimia 80. Kituo hiki ni kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu.
Serikali imeamua kununua dhahabu kutoka kwa Wachimbaji Wadogo kupitia STAMICO ili waweze kuendelea na shughuli zao za uchimbaji pamoja na changamoto ya wanunuzi wa nje baada ya nchi nyingi kufunga mipaka yao kipindi hiki cha Ugonjwa wa Covid-19," Naibu Waziri Stanslaus Nyongo.
Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Singida Chone Malembo amesema Mgodi Mpya wa Kati wa Singida Gold Mine unaomilikiwa na Kampuni ya Shanta Gold Mining Company Limited uliopo wilaya ya Ikungi mkoani Singida umezalisha zaidi ya kilo 49 za dhahabu tangu kuanza uzalishaji mwezi Machi, 2023
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi ameipongeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) kwa kutoa marejesho wa utafiti wa awali unaoonesha uwepo wa madini mbalimbali Wilayani Liwale Mkoa wa Lindi.
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amekutana na Wafanyabiashara wa Madini na Wachimbaji wa Madini kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili kwenye shughuli zao ikiwemo changamoto ya ukosekanaji wa teknolojia ya uchenjuaji wa baadhi ya madini