Kila mtu ana sababu kwanini anafanya kitu fulani. Nikiwa mdogo naenda kuomba 🎤 Club Billicanas walau nionekane , ni mtu ambae ameni inspire kuwa mjasiriamali . Nafsi itanisuta sana nisipo sema kitu . Mimi nimechanga wewe je ? Sina chama , sipendi siasa 🙏🏾
Corona si kitu cha aibu mtu akipata ifichwe, sio ugonjwa wa zinaa useme alieupata alizini kwahiyo iwe siri kumsitiri . Hii ni ya wote , kuweka wazi kunaweza hata kusaidia watu kuchukulia serious na kujilinda zaidi. Mtazamo tu si lazima niwe sahihi.
#staysafe
Ila mimi naimba jamani , Daah!! Yani najisikiliza hapa hata siamini kama huyu ni mimi na hii ni sauti yangu 😂😂😂😂😂😂. Basi watu mtanuna 🙄. Mlitakaje kwani ? Yes i said it 😐
Ukifuatilia maisha ya watu Instagram na ukayatamani unaweza kuiba kumbe hakuna lolote. Sio kila anae post chakula kizuri au mitoko sehemu za maana huwa kalipia yeye mwenyewe. Inawezekana kidogo chako kina amani kuliko maigizo ya watu
Bibi mzaa Mama aliniita ~ Mogondo
Bibi mzaa Baba akaniita ~ Wambura
Baba na Mama wakasema ~ Judith
@ProfessorJayTz
akaniita ~Dada Mkuu
Fans, Dunia na Matukio vikanipa majina kama Komando, Anaconda, Wallet. n.k
Na leo ni siku yangu . 🙏🏾
Hii dhambi ya kuua watu hovyo inachochea chuki sana baina ya watu na watu. Hadi siku atakapouwawa ndugu au mtu wako wa karibu ndio utaujua uchungu wake. RIP kwa wote waliouwawa bila hatia. Hakuna anaestahili kufa kifo cha kinyama. 💔
Uki post uko beach na umevaa nguo za kuogelea watu wanahamaki. Hivi beach tunatakiwa tuvaeje ? Leo nita post. Potelea mbali na shauri zenu 😏😏. Nawaandaa kisaikolojia
Kuna mtu mmoja lazma nimsome Tweet zake ndio nilale. Ngoja niingie nimsomeeee kisha nilale. Usiku mwema, nawapenda wanaonipenda. Wasionipenda mtavuna mlichopanda. ❤️
Nilipost hii TB Instagram watu walicheka sana, naamini walifurahi tu haikuwa kwa nia mbaya, mimi mwenyewe nilicheka. Tunapotoka, tunapokwenda, mabadiliko, na mafanikio zote ni hatua za maisha .
#1998MsasaniBeachDarEsSalaam
Ilikua ni wakati mzuri kusherehekea Bday ya Rais Samia Suluhu
Na ilikua ni heshima kubwa sana kwangu kula nae chakula cha jioni, kukata na kulishwa Cake nae, Na zaidi kukaa meza moja na kuzungumza nae.
#Suluhu
#AmaniNaUpendo
#KaziIendelee
#MamaYukoKazini
Ikumbukwe hata jambazi ana ndugu zake. Acheni kukashifu watu kisa wamempost fulani. Unaweza kunyamaza au kuendelea na biashara zako bila kuzuia wengine wasisikitikie wapendwa wao ambao ni ndugu , jamaa, marafiki au watu wao wa karibu . Je! Sauti inatosha? ,💞
Tuwaheshimu wafanyakazi wa ndani ya nyumba sana . Leo nimesafisha na kupika nahisi mgongo unataka kuchomoka. Usirudi tu huko ukakuta chumvi imezidi ukaanza kugombeza watu hovyo. Kuwa na utu kazi ni ngumu 😐
Poleni sana wasanii wa kike kwa yote mnayopitia, mnayoweza na msoweza kuyaongelea. Nasema tena poleni sana. Sio rahisi kama inavyodhaniwa au kuonekana, mngekuwa wawazi labda ingewasaidia, Mimi huwa naropoka tu liwalo na liwe. Love toka kwa Dada Mkuu ❤️✌🏾
Finally i'm home .
Basi hapo mtanihesabia dhambi ila zenu hamtaziona. Mkimaliza kuhesabu dhambi zangu mniambie. Kumbukeni hata wachungaji wenu wanatumia kwa kujificha bora mimi. Cheers for my son
@IdrisSultan
welcome back. 💞
Nyie watu wa joined May 2020 leo ni siku ya Sabato naomba msinikwaze. Leo sitaki ku block mtu . Nawatakia Sabato njema na kama hupendi mambo yangu tafadhali usini follow . Sio vizuri kujikera nafsi makusudi bila sababu ya msingi. Peace ✌🏾 & Love 💕
Sipendi watu ambao wanajifanya wanataka kupigana halafu hawasogeleani wanasubiri hadi watu wajae waingilie kati wawasukume sukume kuamulia. Mnatunyima uhondo, shikaneni kabla waamuzi hawajaja bana. Show gani hiyo ya kunyoosheana vidole na mikwara ? 😂😂😂😂
Nimemaliza kutengeneza wimbo wa blues nikabaki najiuliza hivi hata nani ataelewa kipindi hiki ? Nikabakia nacheka tu. Basi nita enjoy mwenyewe sio issue.
Hii nazi mliovunja hapa kwangu mngekuna mkaleta tui kwenye plastic container ingenisaidia kuunga maharage. Ila hiki mlichofanya ni uharibifu wa chakula, sijapenda😏.
Kaeni mkijua watu wana njaa na uhitaji. Next time muilete nzima niwafundishe matumizi yake.
Watu msichukulie baadhi ya kazi ni za heshima na kuona mahangaiko ya wengine sio heshima. Kiheshimiwe kinachompa mtu mkate wa kila siku ilimradi sio kuvunja sheria.
Aliewahi kuniuliza kwa dharau ati , what’s your legacy ? Leo nimeishuhudia legacy yake kwa rangi tofauti kabisa 😂😂😂. Nilale kabla sijaharibu. Mdomo JayDee mdomo komaaaaa 🤐
Watu mnaonifahamu msiwe mnanipigia simu usiku mkiwa mmeshalewa baada ya kusikia nyimbo zangu huko mlipo ili watu waone mna ukaribu na mimi wakati you don’t even support my businesses wala shows hamji. Kuweni outsiders tu siwa appreciate wala nini
#FakeAss
😏
Nimefarijika na comments nyingi nzuri juu ya performance yangu ya jana kwenye uzinduzi wa album ya Afro East ya kijana wetu
@harmonize_tz
. Nimefurahi pia kusikia mmeupenda wimbo wetu . Hongera nyingi kwa Harmonize, Muwe na jumapili njema 🙏🏾
Unani follow halafu unaniandikia "Huna maajabu" 😳 Nani alikwambia mimi ni mganga wa kienyeji au mwana mazingaombwe hadi niwe na maajabu? 🤷🏽♀️ Ila watu mnastaajabisha sana 😂😂😂😂
Kabla ya kulala tumuombee kijana wetu mema. Na tumpe pole kwa yote
“🎶 🎼 Idris ukujeeee online, tumeboeka Idris ukuje online tumeboeeka, ukuje tu chatiiii tumeboeka 🎶🎼 “ hako ka wimbo tulikua tunaimba maskini 😢
Gnite people, take care be safe 💕💕
Ukiongea mnafiki, Ukikaa kimya mnafiki. Movement hazina nguvu sababu wanaodhani wamezianzisha wana haki zaidi. Kuna ubinafsi hadi kwenye matatizo? Mtu anataka akianza kuongea wengine wanyamaze? Hapa ndio tunapofeli.
#Ubinafsi
. Tukaneni mkipenda 😏😏
Kuna watu bado wanakutana bar kulewa wakidai maisha lazma yaendelee 🤦🏽♀️🤦🏽♀️ . Hivi ukinunua chupa zako ukanywea nyumbani hutolewa? Au bar napo ni kazini usipoenda hutokula? Mwenye masikio na asikie 👂🏽. Shauri zenu
Nichukue nafasi hii kuwashukuru wote mlionitumia salaam za siku ya kuzaliwa na kunitakia kheri. Nami natuma salaam za upendo kwenu nyote. Nilifurahi sana. Sitatoa wimbo mpya karibuni ila mtapata kuniona kwenye nyimbo nyingi za kushirikishwa hivi punde
#News
Halafu soon nitafanya kitu kingine cha kuwaudhi zaidi ili nikamilishe vizuri maudhi yenu . Mtukane hadi muogelee kisha muone kama kuna litakalobadilika 🙄. Kaeni tayari
Nilichagua kuwa sitaki maisha ya picha bali maisha ya uhalisia kama Dagaa Dagaa kama Kuku Kuku. Kama sina sina , ila sielewi kwanini nikiishi maisha yangu watu mnaniuliza , hata wewe ? Kwani mi nani kwa mawazo yenu? Msinibadili tafadhali . I am who i am 🙏🏾
Leo nimeogopa ku post dinner kwasababu watu wanachukua sahani yangu wanaweka kwao, hivyo nimeamua tulale wote njaa 😂😂😂😂Wazee wa copy & paste leo tunatingisha 🤪
Shetani anapoondoka neema ya Mungu hutawala. Kiuweli nimeiona neema ya Mungu kwa kipindi kifupi sana na sina budi kutoa ushuhuda. Nitatengeneza documentary kushuhudia ukuu wake.