Makampuni ya simu yanapaswa kutoa tamko, kuomba radhi kwa wateja wao na kurejesha bundles zisizotumika ipasavyo katika kipindi cha adha ya internet iliyojitokeza. Kukaa kwao kimya kunaonesha jinsi gani hawajali wateja wao.
Mimi kama mshabiki wa Simba ambaye sina kadi ya uanachama lakini naipenda Simba kufa, sifaidiki kifedha na klabu zaidi ya kufurahia soka safi na ushindi, haijaniteteresha hata kidogo na uteuzi wa CEO mpya, kwangu mimi barida tu. Ninachotaka kukiona na kukisikia ni USHINDI.
Watu wanahoji kwa nini Mbowe hana ulinzi. Tunachotakiwa kuhoji ni kwa nini mtanzania ashambuliwe tu akiwa anaelekea kwake. Kutokuwa na ulinzi hakutoi tiketi ya binadamu kushambuliwa.
Kwa shabiki halisi wa Yanga mwenye uwezo wa kufikiri atajua kuwa this is a very poor management decision by the club. Mtu kawatukana miaka 6 leo unamuajiri 😂 na mnajua kabisa hana mapenzi na nyie isipokuwa pesa, bado mnachekelea, acha mliwe 😂
Vijana wa kitanzania. Unawapa nafasi, unawatafutia connection. Wanabweteka, wanaanza kuzoea, wanajipa ujuaji, wanapoteza uaminifu, wanaanza kutapeli na kuwa waongo waongo. Halafu mwisho wa siku wanaanza kulaumu mablo kuwa wanabana.
Inasikitisha sana kuona Waziri yuko bize akibishana na wananchi mitandaoni kuhusu adha wanayoipata kwa mitandao ya simu badala ya kudili na hiyo mitandao kutatua kero za wananchi. Kuna viongozi wa ajabu sana.
Kuna makundi makubwa matatu Tanzania - yote hujinadi yana mapenzi mema na nchi.
1. Wanasiasa - Usiwaamini
2. Wanaharakati - Chagua wa kuwaamini
3. Wafanyabiashara - Usiwaamini
4. Watu wa dini - Chagua wa kuwaamini
5. Wananchi wa kawaida - Wasikilize sana. Hawa ndio wenye nchi.
Wakati wa Magufuli tuliogopa kutoa maoni mtandaoni kutokana na aina ya utawala wake. Leo tuko na mama Samia, tunaogopa kutoa maoni yetu mtandaoni kwa kuhofia wanaharakati.
Dunia duara.
Utajiri wa nchi, fedha za nchi ni mali ya wananchi. Chama kilichopo madarakani kinatakiwa kusimamia utajiri, kuuendeleza na kusimamia matumizi ya fedha za wananchi na sio kuzifuja au kujinadi kama za kwao.
#Jichague
Nilisoma EGM, Kisha Computer Science. Sasa hivi nafanya mambo ya media, utalii kwa mbali, kukarimu wageni na biashara za hapa na pale.
Maisha hayachagui.
Vipi kuhusu wewe?
Dear Uni students. Yes there is alcohol, sex & drugs. Yes we know u want the life u fantasized when in secondary school. In fact, we totally agree that you've grown up. But also there is career, responsibilities and relationships to build. It's time to add those in the todo list.
It's my daughter's birthday! I am happy and a proud father. This day in 2010, God blessed me with a loving, kind and very smart soul. Thank you for changing my life. I love you Brooklyn-Hope ❤️
Mmepambana, ukweli usemwe. Mmefanyiwa figisu za kufa mtu.
Timu za Tanzania zijifunze namna gani wenzetu Kaskazini wanapambania matokeo, wanacheza ndani na nje ya uwanja, na mashabiki hawako Twitter tu wakibishana, wanaenda uwanjani kusaidia ushindi na silaha za kila aina.
Kuendesha gari Zanzibar unahitaji kuwa na permit, unalipia 10$. Hii ni bila kujali wewe ni Mtanzania au la, we are all regarded as foreigners in this case.
Kuna mtaalamu wa kufix laptops humu? Na kuweka weka zile ma OS na ma drivers na kadhalika? Awe Ni kijana tu hustla, msinipendekezee makampuni makubwa makubwa. Nataka nimuinue hustla mpwa mmoja.
Mwanasiasa: Nakana kuhusika na screenshots za tweets zinazosambaa kunihusu. Zimekuwa fabricated kwa malengo ya kunichafua kisiasa.
Mimi: Tweets ni zangu zina miaka zaidi ya 4 tangu ziandikwe na ndani ya kipindi hicho chote hakuna rangi hatujaona kama watanzania.
NIMEBADILIKA!
On Twitter: "Mama hakosei" "huniambii kitu kuhusu mama" "mama kwanza mke ndio anafuata"
Reality: Demu anahongwa 500K mama anatumiwa 100K tena kwa shida sana, mpaka akohoe damu.
Context: We lie a lot here and the vibe we force to project isn't the reality.
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Haji Manara anaijua kazi yake kuliko mtu yeyote yule. Hakuna msemaji yeyote anayeiweza kazi ya mpira kama Haji Manara.
Pia, lazima kama wana jamii tukiri wazi kuwa hatukuwasimamia vizuri dada zetu
@halimamdee
na
@esteramosbulaya
. Utofauti wa itikadi kisiasa usihalalishe violence against women.
"I'm 33 and at the lowest point of my life. No job, no savings, and the love of my life doesn't love me back. I severely compromised my career because of depression. What should I do?"
- Anonymous
Pia, niliwahi kusema kuwa moja ya makundi ambayo tunapaswa kuwa makini nayo, na kuchagua kwa umakini mkubwa wa kuamini au kutowaamini, ni hili kundi la wanaharakati.
Sio msikilizaji mzuri sana wa redio kwa sasa lakini sidhani kama kuna kipindi kingine cha redio kinachotoa mashavu kwa Bongo Fleva purely, unconditionally, kama Planet Bongo. Kama kipo nifahamishwe. Dullah is the real pioneer of Bongo Fleva wa kizazi cha watangazaji 2010 - 2020.
Last 8
#CAFCL
timu sita kutoka Kaskazini, moja pekee kutoka Kusini na moja pekee kutoka Mashariki ya Africa.
@SimbaSCTanzania
ikiwa katikati ya vigogo Africa. Itoshe kusema Simba ni alama pekee ya soka Africa Mashariki na Kati. Hongera kwa mafanikio haya endelevu 👏👏👏
Kuna ka script kaliandikwa kusapoti tozo. Ma influencers wakatambaa nako weee... Leo kametoka ka script kengine ka "serikali yenu ni sikivu" ma influencer hao hao wanatambaa nako tena.
😂😂😂
Kwa hiyo kumbe Haji alitoa lebo ya mdhamini wa club kwenye press conference? Ndio maana mwanangu MO alikuwa anamuendea direct kwenye post zake. Hii sio sawa kabisa hata kama ni balozi wa maji mengine, bado yeye ni mfanyakazi wa taasisi kubwa ambayo ina ubingwa wa mapinduzi cup.
Zamani, kwenye event za kimataifa, Diamond alikuwa anaonekana kama anashobokea mastaa wengine wa Africa. Sasa hivi kibao kimebadilika. Ukiangalia mastaa wengi Africa ndio wanamshobokea Diamond kwa sasa.
He has earned the power, influence, and status as one the biggest in Africa.
Ulimbukeni wa jamaa zetu:
1. Wanadhani wao ndio wa kwanza TZ kufika fainali ya CAF.
2. Wanadhani wao ndio wa kwanza TZ kufika robo fainali mabingwa Africa.
3. Wanadhani wao ndio wa kwanza TZ kuwafunga wapinzani 5.
Mfano halisi wa kipofu kuona mwezi.
Hangaikeni na hii pia.
Nimefikiria sana cha kuandika nimeshindwa. Itoshe kusema tu hongera sana
@IdrisSultan
umekuwa aggressive sana kwenye kiwanda cha filamu na matunda yanaonekana. Ningesema you are the first Tanzanian to appear on Netflix but Abdu Simba alikuwahi. Si mbaya kuwa wa pili 👊💪
Msemaji wa Yanga anatumia taasisi iliyomuajiri kwa kuamini uwezo wake katika uhamasishaji kufanya personal attacks kwa muajiri wake wa zamani. Aendelee kuishambulia Simba hakuna anayejali ila personal attacks kwa MO is just pathetic!
I haven't made it in life but am fine. I am thankful. I can eat, my kids can eat. My people can eat. We have a shelter. I still have a long way to go towards my goals and dreams. I am not giving up today.
Mtu anithibitishie hapa kwamba wakati wa Magu umeme haukuwa unakatika. Maana yake kwa miaka sita aliyokuwa mkuu wa nchi umeme haukuwahi kukatika.
Nchi gani mlikuwa mnaishi?
MAWAZO YAO:
1. Yeyote mwenye mtazamo tofauti na wao, basi ni mwanachama wa CCM au MATAGA.
2. Wao tu ndio wenye akili na wako sahihi kwa kila wanachofanya - kuliko mtu mwingine yeyote duniani.
3. Wao pekee ndio wanaoitakia mema nchi, sio mtu/chama kingine chochote.
#DuniaDuara
Kijana wa Kitanzania popote pale ulipo, kwenye kazi yeyote ile, kama unapiga kazi kisawasawa na malipo yako hayafurahishi, DAI UNACHOSTAHILI! Kuna ubaguzi sana kwenye hizi ajira ni njaa tu zinawafanya watu wawe kimya.
Hawa hawa vijana wanaomnanga Feisal, ndio walalamikaji wakubwa kwenye ajira zao. Sababu zao ni hizo hizo:
1. Maslahi yasiyoridhisha vs kazi wanayofanya.
2. Manyanyaso kutoka kwa waajiri wao.
Inasikitisha kwamba tatizo hili ni kubwa kwa wengi, sio sekta ya michezo tu.