Tuzo hii ni kwa kila shabiki wa Simba. Kuja kwenu uwanjani kushangilia timu yenu kumeiwezesha timu yetu kushinda Tuzo ya Mashabiki Bora wa AFL. Pongezi nyingi kwenu.
Tumewaletea mchezaji mwingine mwenye uzoefu mkubwa kwenye michuano ya kimataifa. Tunaamini uwepo wake kikosini kwa kushirikiana na wenzake utaleta matokeo chanya.
Kwa kawaida tukiamua jambo letu huwa hatushindwi. Tuwapigie kura
@ClatousCC
au Kanoute ili mmoja wao aweze kuwa Mchezaji Bora wa Wiki wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Kura zinapigwa kwenye ukurasa wa
@CAFCLCC
Katika kipindi hiki focus yetu ni;
1. Kuimarisha benchi la ufundi liwe bora zaidi.
2. Kufanya usajili bora na sahihi, na wa nguvu ili kuiboresha timu yetu iweze kuwa tayari kupambana kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na pia kuendelea kupambana kwenye ligi kuu ili tuchukue ubigwa.
Safari njema kwa kocha wetu Robertinho ambaye amesafiri kwenda nyumbani kwao Brazil kwa shughuli za kifamilia. Kabla mwezi Januari haujaisha atakuwa amerejea kuendelea na majukumu yale.
Malengo yetu ya kushinda ubingwa wa mashindano haya yamekaribia. Hongera kwa benchi la ufundi na wachezaji kwa kazi kubwa ambayo wameifanya hadi sasa.
@simbaqueensctz
Tunataka mwalimu mpya apate muda na wachezaji katika mazingira mazuri kwa ajili ya kuandaa kikosi na michezo iliyo mbele yetu. Kazi ya kuboresha kikosi bado inaendelea. Shukrani za kipekee kwa Rais wa Heshima,
@moodewji
kwa kufanikisha hili.
Ukiacha ushindi ambao timu yetu imepata lakini pia tumetoa Mchezaji Bora wa mashindano, Aquino Corazone na Golikipa Bora wa mashindano, Gelwa Yona. Nawapongeza sana kwa kushinda tuzo hizo.
Leo tunarudi kwenye michuano kimataifa kwa kucheza mchezo wetu wa kwanza ugenini nchini Malawi. Uongozi tumefanya kila kitu kinachotakiwa kwa wachezaji kuelekea kwenye mchezo, tumeongea nao na wao wana ari kubwa kuelekea kwenye mchezo wa leo. Tuwaombee wafanye vizuri.
Nimepata nafasi ya kukutana na Rais wa FIFA, Gianni Infantino alipotutembelea hapa Morocco ambako tunaendelea na kozi ya Diploma katika Uongozi wa Klabu inayotolewa na FIFA (Diploma in Club Management).
Nimefurahi kukutana na Rais wa FIFA, Gianni Infantino pamoja na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu wa FIFA, Ornella Desirée Bellia kujadili kuhusu Super League hapa Park Hyatt jijini Sydney, Australia.
Heshima kubwa kwa timu yetu kutembelewa na Meya wa Kızılcahamam, Süleyman Acar ambaye ndio anasimamia eneo ambalo timu imeweka kambi. Mwanzo wa uhusiano mzuri.
Tumekuwa na mchezo mzuri wa kirafiki dhidi ya Al Dhafra FC hapa Abu Dhabi japo hatujapata matokeo ambayo tulistahili kupata kwa namna tulivyocheza. Nje ya mchezo uhusiano mwema umeanza kati ya timu zetu.
Karibu sana Mheshimiwa Rais Dkt.
@SuluhuSamia
kwenye siku yetu kubwa ya Simba Day. Wanasimba wamefurahishwa na habari hii njema ya kushiriki tamasha letu.
Asante sana ndugu yangu
@moodewji
kwa imani yako juu yangu. Nakuahidi utendaji bora kwenye nafasi hii ili kwa pamoja tuweze kuifikisha
@simbasctanzania
kwenye mafanikio makubwa ambayo inastahili.