TLS is a membership organization that represents Advocates in Tanzania Mainland. TLS is constituted through Tanganyika Law Society Act CAP 307 R.E. 2002.
Wakili Mwandamizi Dr. Mkunga Humphrey Mtingele akimuapisha Wakili Boniface Mwabukusi kuwa Raisi Mpya wa Chama cha Wanasheria Tanganyika katika ukumbi wa Jakaya Convention Center Jijini Dodoma
#TLSAGM2024
Maraisi wastaafu wa
@Tangayikalaw
Mh. Tundulisu na Dkt. Rugemeleza Nshala wakiteta jambo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mr. Charles E. Kichere katika Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika unaoendelea jijini Dodoma.
#TLSAGM2024
Tunaomba radhi kwa taarifa zilizotolewa awali kupitia ukurasa wetu wa X kwamba zoezi la upigaji kura limekamilika.
Taarifa sahihi ni; Zoezi la upigaji kura linaendelea kwa muda wa saa moja kuanzia saa 07:20 mchana hadi saa 08:20 mchana.
Tunaomba radhi kwa usumbufu.
Tukitekeleza
#TLSSection4
, Rais Mwabukusi amekutana na Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi na kujadili ushirikiano hasa katika namna bora ya kuratibu shughuli za siasa nchini kwa kuzingatia mfumo wa demokrasia, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
Leo 20/08/2024, Raisi wa TLS, Wakili Mwandamizi Boniface A. K. Mwabukusi amekutana na kufanya mazungumzo na Sekretariati ya chama hicho. Pamoja na mambo mengine Raisi amejadili na kuweka mikakati ya pamoja katika kuhakikisha malengo ya TLS yanafanyika kwa weledi na kwa wakati.
Kamati maalumu ya TLS suala la
#Ngorongoro
, ikikamilisha mikakati ya utekelezaji hadidu za rejea pamoja na mikakati ya kutembelea maeneo na wadau kwa ajili ya kupata taarifa mahususi ya masuala wanayotakiwa kuyafanyia kazi.
#TLSSection4
#meaningfulengagement
TLS imeshiriki katika kuwasilisha maoni na mapendekezo ya maboresho ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Shule ya Sheria Tanzania 2024, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Kupambana na Rushwa wa Mwaka 2024 na Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya ....
TLS Arusha Chapter iliwakutanisha mawakili wake ktk hafla ya pamoja (WAKILI SOIRE) kujadili masuala ya wanachama & kufarahi pamoja. Rais wa TLS,
@Mwabuk2Boniface
alipewa cheo cha uongozi wa jamii ya Wamasai (LAIGWANANI) kwa mchango wake wa kutetea masuala ya kijamii
TLSSection4
Wanachama wa
@TanganyikaLaw
wanaondelea na Mkutano Mkuu wikitoa heshima zao za mwisho kwa Wakili Maria Pengo aliyeaga dunia mara baada ya kuugua ghafla usiku wa kuamkia leo 2 Agosti 2024.Wakili alishiriki ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa TLS
Roho ya marehemu ilale pahali pema peponi.
Tunapenda kuujulisha umma kuwa TLS inatoa mitazamo, matamko au elimu juu ya sheria kupitia account zake rasmi za kijamii na si account za wanachama wake binafsi. Hivyo chochote anachokipost mwanachama au kiongozi kupitia account binafsi hakifungamani na mtazamo wa
@TanganyikaLaw
Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof. Elisante Gabriel na Mtendaji Mkuu wa TLS Bi. Mariam Othman wakisaini makubaliano kati ya Mahakama na TLS kwa lengo la kuweka utaratibu bora wa kuipatia TLS sehemu ya fedha ambazo zinalipwa na Mawakili Mahakamani kwa mujibu wa sheria.
#TLSSection4
Wakili Mwandamizi Dr. Mkunga Humphrey Mtingele amemuapisha Wakili Emmanuel Ukashu kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa mawakili Vijana wa Chama cha Wanasheria Tanganyika katika ukumbi wa Jakaya Convention Center Jijini Dodoma
Uongozi mpya wa Umoja wa Mawakili Vijana (AYL) chini ya Mwenyekiti Wakili Emmanuel Ukashu umekutana na kujadili masuala mbalimbali kwa maslai mapana ya AYL. Pia kikao hicho kimemkaribisha Rais wa TLS Wakili Boniface Mwabukusi na kumshirikisha mipango yao.
#TLSAYL
#TLSSection4
Rais wa TLS, Wakili
@Mwabuk2Boniface
amesema TLS inatarajia kuwakutanisha wadau mbalimbali kwenye Kongamano la Kitaifa Juu ya Matukio ya Kupotea kwa Raia Nchini Tanzania linalotarajiwa kufanyika tarehe 05 Oktoba 2024.
Video kamili 👇👇
#TLSSection4
According to Section 4 of the Tanganyika Law Society (TLS) Act, the roles and responsibilities of TLS are outlined in detail. These are the key functions of TLS under this section:
#TLSSection4
TLS Kinondoni Chapter, imeendesha mafunzo kwa wajumbe wa Baraza la Usuluhishi ngazi ya kata Wilaya ya Kinondoni. Mafunzo hayo yamewajengea uwezo wajumbe wa mabaraza katika uendeshaji, usimamizi na usuluhishi wa migogoro. Mafunzo hayo yamefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Dodoma: Rais wa TLS,
@Mwabuk2Boniface
akiongozana na Baraza la Uongozi wametembelea Wizara ya
@Sheria_Katiba
na kufanya mazungumzo na Waziri Prof. Kabudi na Katibu Mkuu Eliakim Maswi kujadili masuala ya ushirikiano kwa ustawi wa tasnia na maslahi mapana ya taifa.
#TLSSection4
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Eliezer Feleshi amewaongoza mawakili wanaondelea na mkutano mkuu wa TLS 2024 kutoa heshima zao za mwisho kwa wakili Maria Pengo aliyeaga dunia mara baada ya kuugua ghafla usiku wa kuamkia leo tarehe 02 Agosti 2024.
Letter from TLS President, Fatma Karume - Law Day 06th February 2019
Please receive a letter from
@TanganyikaLaw
President, Ms.
@fatma_karume
in respect of the Law Day that will be celebrated tomorrow, 06th Feb 2019.
Follow the link for attachment ===>
Tunapenda kuwashukuru wanachama wa
@TanganyikaLaw
kwa kushiriki katika Uchaguzi wa Viongozi, Matokeo ya Nafasi ya Raisi wa Tanganyika Law Society
Edward Hoseah 621
Harold Sungusia 380
Jememaih Mtobesya 145
#2022TLSAGM
TLS mkoa wa Kinondoni iliwakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali kujadili changamoto zinazowakabiri mawakili na namna bora ya kuzitatua. Kikao kazi hicho kilifanyika tarehe 24 Agosti 2024 katika ukumbi wa Wakili House jijini Dar es Salaam.
Announcing to you the New Governing Council of
@TanganyikaLaw
for the year 2019-2020 as follows
PRESIDENT- RUGEMELEZA NSHALA
VICE PRESIDENT- MPALE MPOKI
HONORARY TREASURER -NICHOLAUS DUHIA
#TLSAGM2019
TLS imewakutanisha pamoja wadau mbalimbali nchini kujadili miswada ya sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Sheria ya Tume ya Uchaguzi ya Taifa pamoja na Sheria ya Vyama vya Siasa. Mjadala huu unafanyika jijini Dar es Salaam leo tarehe 15/12/2023.
Waziri mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba (mgeni rasmi) akizindua kitabu cha Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta, tukio lililofanyika kwenye ukumbi wa Wakili House Dar es salaam na kuhudhuriwa na majaji na wageni mbalimbali.
TLS yashinda kesi ya Kikatiba dhidi ya Serikali ya Tanzania iliyofunguliwa mwaka 2014 kupinga azimio lililoafikiwa na Serikali ya Tanzania la kulizuia Baraza la Jumuiya ya SADC kuamua kesi kutoka kwa wananchi wa nchi wanachama wa SADC.
Tunaendela na Mkutano Mkuu wa
@TanganyikaLaw
ambao utamalizika kesho kwa uchaguzi wa viongozi wapya wa chama. Mgeni rasmi katika mkutano huu ni Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Sammata
@TLSAGM2019
Hii sio sahihi kabisa! wanafunzi hawa wanawahi shule, dereva yeye ameshachukua tahadhari kwa kuvaa kofia ngumu. Bodaboda kwa sasa zimekuwa ni usafiri wa umma. Ni vyema tupitie sheria yetu ya usalama barabarani ili iwe ni lazima kwa abiria wote kuvaa kofia ngumu
#Ajalisasabasi
.
Mkurugenzi Mtendaji wa
@TanganyikaLaw
Bi. Mariam Othman akikabidhiwa zawadi na mgeni rasmi Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Dotto Bitteko wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu.
#TLSAGM2024
Baraza la Uongozi TLS likiongozwa na rais Boniface Mwabukusi na Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof. Elisante Gabriel wametembelea jengo kuu la Mahakama (JUDICIARY SQUARE) linaloendelea na ujenzi kujionea miundombinu yake hasa upande wa TEHAMA.
#TLSSection4
Ni vizuri watunga sheria wawe objective na wakumbuke hawatadumu kwenye nafasi zao milele ukitunga sheria kwa kukandamiza watu kesho itakugeukia wewe ukishapoteza dhamana kwa hiyo tuwe waungwana - Sungusia Harold
#WikiYaAZAKI2018
Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma Mhe. Edwin Kakolaki akiwapokea Baraza la Uongozi TLS na Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof. Elisante Gabriel wakati walipotembelea Mahakama Jumuishi na kujionea utendaji kazi wake hasa kwenye mifumo ya TEHAMA.
#TLSSection4
Mwendokasi ni sababu kuu katika nusu ya vifo vitokanavyo na ajali za barabarani: Unga mkono serikali katika marekebisho ya sheria ya usalama barabarani yenye vipengele vinavyopunguza viwango vya mwendokasi nchini kote.
#Ajalisasabasi
#ChangeTanzania
#monda
Marekebisho yaliyopendekezwa katika sheria ya usalama barabarani ya mwaka 1973 yanahitaji wasafiri wote wa mbele na wa nyuma kufunga mikanda yao ya kiti ili kupunguza athari zinazosababishwa na ajali za barabarani: Unga mkono serikali katika kupitisha sheria hii.
#Ajalisasabasi
Wakili Mwandamizi Mpale Mpoki akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Sakata la Kufungiwa Uwakili kwa miezi 6. Aeleza hatua ambazo anazichukua juu ya sakata hili. Fuatilia mahojiano yote kupitia link hapa chini
Wajumbe kutoka Chama Cha Wanasheria nchini China wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi bwana Wang Wei wameitembelea
@TanganyikaLaw
na kukutana na Rais
@fatma_karume
pamoja na Uongozi wa Secretariet lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji!
Chama cha Mawakili Tanganyika kinampongeza wakili Harold Sungusia kwa kuchaguliwa kuwa Raisi wa Tanganyika Law Society kwa mwaka 2023-2024 kwa kupata kura 748 kati ya kura 825
#TLSAGM2023
Mitindo mingine ya nywele za dada zetu hairuhusu helmet kukaa vizuri kichwani kitu kinachoongeza athari wakati wa ajali. Hata hivyo sheria yetu ya usalama barabarani haiwalazimishi abiria wa boda boda kuvaa kofia ngumu. Tumeendaa mapendekezo ya kuboresha sheria hii ya tangu 1973
Simu inaweza kusubiri ila ajali haitasubiri. Pamoja na kuwa matumizi ya simu yameongezeka,
#Tanzania
bado hatuna sheria inayosimamia matumizi ya simu kwa madereva.
@TanganyikaLaw
na wadau wengine tumeliona hili na tunalifanyia mchakato. Tuungeni mkono.
#AjaliSasabasi
Ziara ya
#TLSSection4
inaendelea na hapa TLS inapokelewa na Mkurugenzi wa Ofisi ya Mashtaka ya Taifa Silvester Mwakitalu na kuzungumza namna ya mawakili wa serikali na binafsi kushirikiana katika kuendesha mashauri ili kuisaidia mahakama kuamua kwa haki na mujibu wa sheria.
Uchambuzi wa Kisayansi kuhusu Azimio na Nia ya Tanzania kujitoa katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Watu na Binadamu kupitia Ibara ya 34(6) ya Itifaki ya Mkataba Unaoanzisha Mahakama ya Afrika. Wataalamu, & Wadau mbalimbali wametoa maoni yao. Nasi Tutayakilisha
@Sheria_Katiba
TLS inatambua uwepo wa mijadala inayoendelea nchini kuhusu makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kuhusu uendeshaji wa bandari ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Falme ya Dubai...
Pombe ni hatari kwa dereva hivyo ni muhimu kuchagua moja kuendesha chombo cha moto au kulewa! Tupo kwenye mchakato wa kushawishi maboresho ya Sheria ya usalama barabarani ili kuthibiti matumizi makubwa ya vilevi kwa madereva. Tunaomba mtuunge mkono.
#AjalisasaBasi
TAMKO KUUNGA MKONO JUHUDI ZA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI JUU YA HAKI YA MTUHUMIWA KUPEWA DHAMANA KATIKA KITUO CHA POLISI
Rais
@fatma_karume
atoa tamko kwa niaba ya Baraza la Uongozi wa
@TanganyikaLaw
. Bonyeza hapa kudownload =>
Kiongozi wa TLS Kanda ya Kati Laetitia Petro ameongoza jopo la mawakili waliokuwa wakimtetea mjane Maria Ngoda aliyehukumiwa kifungo cha miaka 22 jela kwa kukutwa na nyama ya swala na kushinda rufaa hiyo kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Iringa.
IT'S TOMORROW!
TLS, in collaboration with Haut- Katanga Bar Association- from Congo DRC has organized a match between *WAKILI FC* and *CS BALANCE, a team from Congo DRC- HK Bar.
The match will take place tomorrow at the Law School of Tanzania from 9:00 am!
Raisi wa
@TanganyikaLaw
@fatma_karume
azungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kukamatwa kwa mawakili na kuwekwa ndani kinyume na sheria wakati wakiteleza majukumu yao ya kazi.
"Some people come into our lives, leave footprints on our hearts, and we are never the same." Our Condolences to
@CloudsMediaLive
, Ruge's family and Tanzania in general.
#RestinPeaceRuge
Ukiwa umefunga mkanda utapunguza madhara ya ajali kuanzia 50% kwa abiria wa kiti cha mbele na 70% kwa abiria wa viti vya nyuma. Changamoto ni sheria mama inayosimamia masuala yote ya barabarani haisemi lolote kuhusu kufunga mkanda kwa abiria wa viti vya nyuma.
#Ajalisasabasi
Mawakili wapya wakitoa heshima kwa CLE(Council for Legal Education) wakati wakiapishwa. Mawakili 549 wamepokelewa na Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
@TanganyikaLaw
tunasema Karibu Sana!
RAISI WA TLS FATMA KARUME AHUDHURIA KIKAO CHA TATHIMINI "POST SESSION MEETING" CHA MAHAKAMA YA RUFANI.
Kikao kinaendelea, wadau wengine wa mkutano huo ni Mwanasheria Mkuu, Mkurugenzi wa Mashtaka, Mwanasheria wa Serikali Mfawithi, Mkuu wa Gereza na Afisa wa Polisi Kanda Maalum.
Wanasayansi wa mambo ya siasa pamoja na wananchi wameudadafua mswada wakiutazama kwa jicho la namna gani wananchi wataathiriwa na mswada huu iwapo utapitishwa. Wanaitaka serikali/bunge iyachukulie chanya mawazo yatakayowasilishwa na iyafanyie kazi.
#MuswadaWaVyamaVyaSiasa
#MuswadaWaVyamaSiasa
pia tutakuwa live kupitia account zetu ambazo ni tanganyika law society(facebook) na hapa tweeter! huku shangazi akionekana kuvutiwa na mjadala wa kesho. Si ajabu ataurusha live kupitia account yake ya
@fatma_karume
Chama na Mawakili nchini
@TanganyikaLaw
wameandaa mjadala Kuhusu Muswada wa Sheria ya Vyama vya Siasa. Ninawapongeza sana kwa uamuzi huu kwani utaongeza uelewa zaidi wa umma Kuhusu muswada huu kandamizi. Kesho asbh Kisenga Hall, Millenium Towers, tukutane kujadiliana
Baraza la uongozi
@TanganyikaLaw
likiongozwa na Rais wake wakili Harold Sungusia
@haroldsung_
wakimkabidhi zawadi Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Dotto Biteko kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu.
#TLSAGM2024
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimeandaa kongamano la wazi kujadili "Namna Bora ya Kuhuisha Mchakato wa Katiba Mpya" ambapo zaidi ya watu 350 kutoka Tanzania nzima, wadau mbalimbali pamoja na wananchi watashiriki.
WAKILI FC YA TLS YAIBUKA KIDEDEA DHIDI YA CS BALANCE YA CONGO DRC ( 5 -0)
Mechi ya kirafiki imechezwa katika uwanja wa Law School, Dar. TLS inawashukuru mawakili kutoka Congo DRC kwa kuthamini mahusiano na kuitembelea TLS na ZLS ya Zanzibar
Chama cha Mawakili Tanganyika kinampongeza wakili Edward Heche kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Mawakili Vijana(AYL) wa TLS kwa mwaka 2023-2024
#TLSAGM2023
Je! Wajua sheria ya usalama barabarani ya mwaka 1973 haimlazimishi abiria wa boda Boda kuvaa kofia ngumu? inamtaka dereva tu kuvaa kofia ngumu. Tupo kwenye mchakato wa kushawishi maboresho ya Sheria hii kwa sababu Boda boda kwa sasa umekuwa ni usafiri wa umma.
#Ajalisasabasi
TAMKO LA TANGANYIKA LAW SOCIETY (TLS) JUU YA UAMUZI WA KAMATI YA MAWAKILI KUMUONDOA BI. FATMA AMANI KARUME KATIKA REJISTA YA MAWAKILI TANZANIA BARA NA UAMUZI WA WAKILI FATMA AMANI KARUME KUKATA RUFANI
Rais wa TLS Dr. Rugemeleza Nshala (wa kwanza kulia) akiwa na majaji wastaafu pamoja na wageni waalikwa kwenye uzinduzi wa kitabu cha SUPREMACY OF LAW kilichoandikwa na Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta uliofanyika ukumbi wa Wakili House.