TUNAREJESHA: TAKUKURU (W) ya Misungwi - Mwanza imeokoa na kumkabidhi Bi. Teddy Barongo (52) King'amuzi cha Azam, kochi na solar power mali ambazo alinyang'anywa na Kampuni ya ukopeshaji ya ZANE MICROFINANCE ya jijini Mwanza. - Februari 20, 2021.
TUNAELIMISHA KUTOKA RUNGWE (MBEYA). "Muwe mstari wa mbele na tayari kushirikiana na TAKUKURU katika mapambano dhidi ya Rushwa mara mtakapomaliza mafunzo yenu na kuelekea katika vituo vyenu vya kazi".Februari 07, 2023.
WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI ILOPA WAELIMISHWA KYELA-MBEYA"Ipende nchi yako kwa kutokutoa wala kupokea rushwa, kwani rushwa ni adui wa haki". Hayo yamesemwa na Afisa wa TAKUKURU Bi. Jovinatha Firberty, Februari 13, 2023.
Watumishi wanawake wa ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Mara wametembelea Kituo cha kulelea Watoto Yatima cha Musoma Children Home na kutoa mahitaji mbalimbali katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2023.Maadhimisho Hayo yamefanyika kimkoa wilayani Musoma.Machi 08, 2023
RUSHWA YA NGONO ISIWE KIKWAZO CHA KUPATA AJIRA: "Watumishi wenye mamlaka tumieni nafasi zenu vizuri na mtende haki pale inapostahili bila kuhitaji upendeleo wa kingono."Bi. Maua Ally wakati alipokuwa anaelimisha jamii kuhusu madhara ya rushwa ya ngono kupitia Februari 01, 2023.
Pichani ni Hamadi Maarifa, wanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Toledo akielezea namna tamaa ya mali inavyoweza kumfanya mtu kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu na uaminifu na hatimaye kujihuaisha na vitendo vya rushwa. TAKUKURU TANGA 19/10/'23.
TUNAELIMISHA:
Afisa Uchunguzi Rajabu Said wa TAKUKURU wilaya ya Kibiti mkoa wa Pwani akitoa Elimu Dhidi ya Rushwa kwa wanachama wa Klabu ya Wapinga Rushwa Shule ya Msingi Kingunguli - Kata ya Mwambao - Septemba 29, 2020.
TAKUKURU RAFIKI NA HUDUMA BORA KWA WANANCHI- MISUNGWI MWANZA: Pichani ni wawakilishi wa Wananchi na wadau wa Kata ya Kanyelele wakieleza kero zao kwa matumaini ya kupata huduma bora za kijamii na miradi ya maendeleo yenye tija kwa manufaa yao na vizazi vyao. Februari 17, 2023.
*TUNAELIMISHA* :
Pichani ni Mkuu wa Dawati la Elimu kwa Umma TAKUKURU (W) ya Mbulu-Manyara, Christopher Mbano (Wa kwanza kulia waliokaa), katika picha na Viongozi wa Kamati za Watumiaji Maji - H/W ya Mbulu, baada ya uelimishaji kuhusu RUSHWA NA MADHARA YAKE, Oktoba
30, 2021.
TUMEREJESHA:
Kaimu Mkuu wa TAKUKURU (M) wa Arusha James Ruge, ameuhabarisha umma kuhusu utendaji kazi wa ofisi yake kwa kipindi cha Aprili-Juni 2020 uliohusisha kuokoa kodi ya Serikali kutoka Kampuni ya Kitalii ya Eshkesh na Chama cha Ushirika ACU ya zaidi ya sh Bilioni 1.76.
WANAFUNZI S/S MBINGA DAY WAELIMISHWA JUU YA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA: "TAKUKURU ina uhusiano mkubwa sana na mahakama katika kukemea vitendo vya rushwa kwani yeyote anayethibitika kutenda kosa la rushwa hufikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka kulingana na kosa alilolitenda"
KLABU YA WAPINGA RUSHWA S/S KILYABOYA YAFUNGULIWA- KWIMBA MWANZA:"Kuweni wazalendo na muichukie Rushwa katika maisha yenu"Fidelis Kinyamagoha akieleza wanafunzi kuhusu umuhimu wa kujiunga na klabu ya wapinga rushwa na lengo la kuanzisha Klabu za WAPINGA rushwa.23/2/23.
TAKUKURU (W) MISSENYI yatoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa kwa madereva wa bodaboda waliofika ofisini hapo. Madereva wa bodaboda wamehimizwa kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa za vitendo vitendo vya rushwa TAKUKURU.6/2/'23.
RADIO SAFINA Kaimu Mkuu wa TAKUKURU (M) ARUSHA Bi Zawadi Ngailo amewaeleza wananchi wa Mkoa wa Arusha kuwa “Ni wajibu wa kila mwananchi kuzilinda na kuzithamini rasilimali za Taifa,kwani kwa kufanya hvyo itapunguza swala zima la ubadhirifu wa mali hizo kwa kiasi kikubwa”.5/6/23.
TUNAELIMISHA: JESHI LA POLISI KWIMBA- MWANZA. Askari wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza wakumbushwa umuhimu wa kuzingatia maadili na kuepuka vitendo vya rushwa katika utekelezaji wa majukumu yao. TAKUKURU Mwanza,Disemba 21, 2022.
*TAKUSKA* *NGAZI* *YA* *WILAYA* - *MWANZA* : Pichani mbele ni Mkuu wa TAKUKURU (M) Mwanza, FRANK MKILANYA, akizungumza na Wakuu wa TAKUKURU Wilaya na Maafisa wa Madawati ya Elimu, kuhusu MWONGOZO WA WAWEZESHAJI WA KUFUNDISHA VIJANA WA SKAUTI KUHUSU KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA.
*TUNAHABARISHA* . Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tabora Bw. Musa Chaulo, ameuhabarisha umma kuhusu utendaji kazi wa TAKUKURU Mkoa wa Tabora, kwa kipindi cha Julai - Septemba 2021. Ameeleza wamekagua miradi 13 yenye thamani ya shilingi 4,780.498,736.71 na kutoa ushauri.
TAKUKURU KILIMANJARO YAWAFIKIA MTAA WA NG'AMBO "Msikubali mriradi iliyoletwa na Serikali kama ya ujenzi wa shule kama iliyopo hapa ikajengwa chini ya kiwango wakati mnaona. Toa taarifa ili tudhibiti ubadirifu mapema..."Yalisemwa hayo na Afisa wa TAKUKURU , *Disemba 22, 2022.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama (Mb), leo Februari 9, 2022 atembelea Taasisi ya Kuzuia na Kumbana na Rushwa - TAKUKURU na kukutana na Menejimenti pamoja na Watumishi wa TAKUKURU
*TAKUKURU* *INAYOTEMBEA* : Pichani ni Mkuu wa Dawati la Elimu kwa Umma TAKUKURU (M) wa Rukwa - Musa Gyunah, akijibu kero za wananchi zinazotokana na vitendo vya Rushwa, katika Mkutano uliyofanyika Oktoba 28, 2021, Kijiji cha Mtowisa, Sumbawanga, kupitia TAKUKURU INAYOTEMBEA .
WAAJIRIWA WAPYA KAKONKO WAASWA KUJIEPUSHA NA RUSHWA. Waajiriwa wapya katika Idara ya Afya, Elimu, Utawala na Kilomo - Wilaya ya Kakonko wameaswa kutojihusisha na vitendo vya rushwa katika utumishi wao ili kudumisha Imani ya wananchi kwa Serikali yao. Disemba 16, 2022.
TAKUKURU RAFIKI YAWAFIKIA MADIWANI KINONDONI Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni Bw. Ismail Seleman amewaelimisha Madiwani wa Manispaa ya Kinondoni kuhusu Programu ya TAKUKURU RAFIKI na mapambano dhidi ya rushwa wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani. Februari 22, 2022
TAKUKURU (W) KALAMBO YAIMARISHA KLABU YA WAPINGA RUSHWA S/M SENGAKALONJE"Ili muweze kujenga jamii bora na yenye maendeleo mnatakiwa kuwajibika katika kukuza uelewa wa mapambano dhidi ya rushwa kwa jamii inayowazunguka."Afisa wa TAKUKURU Bw.Simbeye.TAKUKURU Rukwa Aprili 21, 2023.
Katika picha ni wadau wa mazao yatokanayo na misitu baada ya warsha iliyofanyika ofisi za TAKUKURU Songea. Katika warsha hiyo, wadau wamejadili na kuweka maazimio ya kudhibiti rushwa katika utekelezaji wa majukumu yao. TAKUKURU Songea, Mei 19, 2023.
KONDOA GIRLS YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO TAKUKURU ARUSHA: Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kondoa (KONDOA GIRLS), wamefanya safari ya kimafunzo katika ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Arusha na kujifunza kuhusu rushwa na athari zake. TAKUKURU Arusha, Disemba 19, 2022.
Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Jijini Arusha yametoa fursa kwa TAKUKURU kuelimisha makundi mbalimbali kuhusu Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.Pichani ni Afisa wa TAKUKURU Mkoa wa Arusha Bw.Reuben Maduhu akitoa elimu hiyo kwa wanafunzi wa Shule ya MSINGI Naurei.24.1.2023
Wanafunzi wanachama wa Klabu ya Wapinga Rushwa Shule ya Sekondari Namichiga iliyopo wilayani Ruangwa wakisoma taarifa ya klabu yao mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge Bw. Abdalla Shaib Kaim wakati Mwenge wa Uhuru 2023 ulipotembelea Klabu hiyo.TAKUKURU Ruangwa, Aprili 12, 2023.
TAKUKURU RAFIKI - UTAMBUZI WA KERO KATA YA KASOLI, BARIADI Afisa wa TAKUKURU Bw. Jaji John Zakaria akikusanya karatasi zilizoandikwa kero mbalimbali katika kikao cha utekelezaji wa Programu ya TAKUKURU RAFIKI kilichofanyika katika Kata ya Kasoli. TAKUKURU Simiyu. Februari 17,2023
Pichani ni Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Arusha (kulia) akipokea machapisho yenye ujumbe wa PROGRAMU ya TAKUKURU RAFIKI kutoka kwa Afisa wa TAKUKURU Mkoa wa Arusha Bi.Mariam Yusufu ikiwa ni mwendelezo wa kuitambulisha Programu hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Arusha.17/01/2023.
PROGRAMU YA TAKUKURU RAFIKI YATEKELEZAA SONGWE Katika picha ni Afisa wa TAKUKURU Bi. Lilian Matara (aliyesimama), akisaidia Mdau wakati wa uibuaji wa kero katika utekelezaji wa Programu ya TAKUKURU RAFIKI Kata ya Nambinzo Wilaya ya Mbozi.Machi 23, 2023
MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na mahakimu wa Mahakama ya Kanda ya Mbeya wametembelea Gereza la Songwe Mbeya kwa lengo la kusikiliza kero na kuwapa wafungwa elimu ya Rushwa. TAKUKURU Mbeya. Januari 26, 2023