Maisha ya mtandaoni ni kama fuko la taka yaani unaweza kung'ang'ana kumwelewesha mtu kuhusu kanuni fulani za maisha kwa nguvu zote na haelewi kumbe ni mtoto wa kidato cha pili yuko bwenini ila ana simu janja tu.
Nimetoa top yake, akanyamaza. Nimetoa bra, akanyamaza. As I was trying to remove her pant akashout, "Hey jirani! Unamaanisha hio nafasi haitoshi kuanika blanket yako?" Nimerudi na nguo zangu kwa hiyo nikaamua ntazianika kesho. Wewe endelea kuoza akili! 😂😂😂
Ukiwa mstari wa mbele kusaidia wagonjwa wa korona. Hakuna kitu kinavunja moyo na kuua morali wa kazi kama kutopata posho na vitendea kazi kwa wakati. 😇
Kampuni la Baiteknolojia toka Israeli limedai limepata dawa ya virusi vya korona inayotibu kwa 100% imetibu watu kadhaa walikuwa mahututi na sasa imepelekwa Marekani kwa majaribio zaidi.
#TibaFasta
Ukiaangalia TBC 1 kila kinachoonyeshwa haipiti dakika bila kumshukuru Rais. Na hakuna mwenye mawazo mbadala yaani kila kitu PERFECT tu. Kweli tuko vizuri. Televisheni imekuwa ya chama kabisa sio ya taifa tena.
Zamani kidogo, nyumba nzuri zikiwa zinajengwa mtaa mmoja utaambiwa za Ridhiwani, yakipita magari makubwa yanayofanana ya Ridhiwani, ikijengwa hoteli kali ya Ridhiwani yaani kila kitu kizuri cha Ridhiwani. Kweli kila zama na mambo yake! 😂😂😂
Mchungaji kaona simu yangu niliyonunua laki 5, akasogea & kuniuliza kwa upole nimenunua bei gani, kwakuwa natoaga sadaka kidogo nikamjibu nimenunua elfu 50. Akanipa laki 1, nikanunue 2, yake & ya mke wake. Sasa ndio namuuliza Mungu kwanini kaamua kuniadhibu mbele ya mchungaji! 😂
Heka moja ya matikiti ina uwezo wa kutoa matikiti 10,000 ambapo kila tikiti ukiamua kuuza kwa bei ya haraka ni 2,000 Tshs kwa hiyo ukichukua idadi ya matikiti 10,000 X 2,000 Tshs =20M ukitoa laki 4 za uzalishaji unabakiwa na 19.6M. Kilimo cha kwenye makaratasi rahisi sana. 😂😂😂
Ili kuongeza uwezekano wa kupata mtoto wa kiume inapaswa kufanya tendo la ndoa kwa mtindo ambao unaruhusu uume kuingia ndani zaidi (deep penetration) kitu kitakachorahisisha mbegu kufika haraka kwa yai.
#ElimikaWikiendi
Ukiwa umeshiriki ngono bila kinga na mtu na ukafahamu ana VVU kama bado ndani ya masaa 72 unaweza kupata dawa zitakazo kukinga na VVU katika kliniki zinazotoa huduma za afya kwa watu wanaoishi na VVU.
#ElimikaWikiendi
Mabinti wa kiafrika, mnapendeza zaidi na hizo nywele na ngozi zenu za asili, msijitie na kututia gharama zisizo na mpango kununua mawigi na vipodozi vya kujichubua. 😂
Punyeto inaweza kumsaidia mtu kuondoa mkazo (stress), kuboresha hali (mood), kumsaidia mtu kupata usingizi, huongeza umakini (concentration) na ufanisi katika tendo la ndoa n.k!
#ElimikaWikiendi
Huyu jamaa anajua Kiingereza cha kuombea maji kaniaomba selfie, kimsingi hajawahi kukutana na mwafrika hata haijui
#Afrika
. Ana taaluma ya uhandisi, sijui shule ya msingi hawafundishwi Jiografia ama ramani ya dunia. Wakati niko shule ya msingi naijua dunia nzima Kwa Atlas! 😂😂😂
Maumivu ya kufunga ndoa na mtu asiyefaa ni makali kuliko hofu ya kuzeeka bila mwenza wa maisha. Ndoa sio mashindano, tumia muda wa kutosha kusitawisha sifa bora na kuzitafuta kwa umpendae kabla ya kufanya maamuzi mazito. Ni bora kusubiri muda mrefu kuliko kukurupikia asiyekufaa.
Nilipokuwa mdogo nikiwa Kahama nilitamani sana kwenda Dar es Salaam, nilipokuwa mkubwa nikatamani New York, Mungu si Athumani pote nimefika sasa natamani kwenda "Mbinguni" tu ila sio kufa sasa hivi. 😂😂😂
Wapwa kabla ya kubanjuka kavu kavu siku hizi kuna vipimo vingi mno vya kupima VVU kwa haraka na uhakika, kuna vingine unapima kwa mate tu na kinakupa majibu chap. Kama hakuna vipimo ni bora kutumia kinga.
#WapwaTuinuane
Kuna mhindi mmoja kanikosha sana kwenye ndege, mhudumu kaenda na kiingereza kingi kwa yule mzee. Mzee akamjibu ongea lugha ya taifa mie sielewi lugha zenu. Mie woyoo,
#Kiswahili
oyee! Chiii! 😂😂😂
Hello beautiful people. I thank Jehovah God to be awarded a Commonwealth Scholarship
@commschols
funded by the Department of International Development
@DFID_UK
to study a Master of Public Health (MPH) at The University of Manchester
@OfficialUoM
"Wenye ideas hawana capital, wenye capital hawana ideas, trade your ideas to the people with capital and get partnership into practice." ->
@MarekaMalili
Kuna wakati unaomba kazi hadi unakata tamaa kumbe kwenye CV yako umeandika wewe ni MD au CEO wa kikampuni chako sasa HR anaona unatafuta kazi ya nini? 😂😂😂
Wanawake wanene au wenye uzito kupita kiasi au waliozaa huwa na matumbo makubwa au vitambi vinavyoharibu muonekano wao mzuri. Ili kuwa na tumbo zuri (flat belly) bila ya kuwa na mtaalamu wa mazoezi (waist trainer) fuatilia huu uzi (thread).
#TibaFasta
Vyakula Vinavyoongeza Uwezo wa Kujamiana: Nguvu na nyege ni muhimu katika kufurahia tendo la ndoa, maparachichi yanaweza kukupa vyote viwili. Maparachichi yana madini, mafuta (yanayolinda moyo na kupunguza lehemu) na vitamin B6 ambavyo vyote hukupa nguvu na nyege.
#TibaFasta
Siku nyingine ukiona kodi ya pango inakaribia ukingoni, mfuate mwenye nyumba muombe akukopeshe hela ili umlipe kodi yake. Mbaki mnadaiana madeni ya kawaida! 😂😂😂
Leo nimeamka alfajiri nifanye jogging kidogo nikakumbuka maandiko ya Biblia Methali 28:1 ~> "Muovu hukimbia hata asipokimbizwa" Nikaamua kurudi kulala. Neno la Mungu ni la kuheshimu sana! 😂😂😂
Mmoja wa wafiwa alitembelea Ofisi za Manispaa ya Ilala, akaona kitabu cha "Mazishi ya
#COVID19
" na marehemu baba yake alikuwa namba 256. Kama ni Ilala tu hiyo basi tutaisha kimya kimya.
#COVID19TZA
#COVID19Tanzania
I am so proud of my university, The University of Manchester
@officialUoM
which is working towards developing a test for COVID-19 that could be used at home like a domestic pregnancy test.